Wakala wa Wayne Rooney aenda China kujadili uhamisho.


Isaac Classic Bdi







Wakala wa Wayne Rooney Paul Stretford yupo nchini China kufanya mazungumzo kujaribu kuona iwapo atafanikiwa kuhamia klabu ya Ligi Kuu ya China.
Bado hakuna hakikisho lolote la mafanikio na duru zinasema huenda ikawa vigumu kwake kufanikiwa kuhamia huko kabla ya muda wa wachezaji kuhama China kumalizika tarehe 28 Februari.
Lakini hali kwamba Stretford amesafiri China ni ishara wazi kwamba meneja wa Manchester United Jose Mourinho anaweza kumwacha Rooney, 31, ahame.
Na iwapo hatafanikiwa kuhama mwezi huu, basi bila shaka atahama majira ya joto.
Rooney ameshuka hadhi United chini ya Mourinho na amekuwa hapati nafasi ya kuanza kwenye kikosi.



No comments